Wednesday, June 11, 2014

SHILOLE MAHABA YAMEMLIPUKIA

                                        SHILOLE A.K.A SHISHI BABY
TATOO YA BOYFRIEND WA SHILOLE

Kwa hivi sasa hakuna asiyejua kwamba muigizaji mwenye mafanikio na mtafutaji na mwenye akili ya maisha SHILOLE anamahusiano na Serengeti boy wake ambaye ni mwanamziki wa kizazi kipya Nuhu Mziwanda, basi bwana licha ya kwamba Nuhu kiumri ni mdogo kwa Shilole lakini kijana huyo kawaonyesha mijibaba isiyojua kupenda na inayojua kuumiza mioyo ya waschana jinsi ya kupenda, kwanza kijana huyu unaambiwa anampenda shilole kupita maelezo, wako wote kama kumbi kumbi lakini kijana kaenda deep zaidi pale alipoamka na kuamua kwenda kuchora TATOO yenye jina la A.K.A ya Shilole ambayo ni Shihi babe, kijana hataki mchezo kabisa, pia ikumbukwe Shilole anawatoto wawili lakini kijana kaamua kumpenda shilole na watoto wake pia,

ANGALIZO.... Tatoo ni mchoro usiofutika na ukiweza kuufuta basi utabaki na kovu, kwa kua haufutiki watu huwa wanafikiria mara mbili mbili kwanza kitendo cha kuamua tu kujichora tattoo mwilini, wakishaamua kwamba wako tayari kujichora wengi huwa wanajichora picha zenye maana kubwa maishani mwao, au majina ya baba na mama au ya watoto wao, KWA NUHU KACHA KUCHORA JINA LA MAMA AU LA BABA YAKE NA KUAMUA KUCHORA LA SHILOLE TENA LIMEENEA MKONO MZIMA NAMUOGOPEA, kwasababu huyu kijana bado mdogo, huko mbele kuna mabadiliko mengi tu yamaisha yanakuja kwa hyo unaweza ukaishia kuoa mschana mwingine kabisa, au pia ya Mungu mengi unaweza ukaishi na Shilole mpaka uzeeni then hapo itakua afadhari, lakin ikitokea mmeachana je hyo Tatoo utaifanyaje, na ikitokea Shilole ndo kaamua kukuacha na kua na mwanaume mwingine itakuumiza sana na utaumia kila unapoangalia mkononi hiyo tattoo, ungeweza kuonyesha unampenda kwa njia nyingi lakin kwa tattoo umekwenda mbali sana we bado mdogo sana I hope hautakuja kujutia hili swala.
SHILOLE HONGERA KAKIJANA KA HANDSOME .



No comments: