Thursday, June 19, 2014

KUHUSU MUIGIZAJ LULU KUZICHAPA NA WALIYEIBIANA NAE BWANA HUSNA, INGIA USOME HUMU






MASTAA wa kike wanaotingisha Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ (pichani)  na Husna Maulid, ilibaki kidogo wazichape, Amani lina mchapo mzima



Kabla ya tukio hilo, awali wawili hao waliwahi kuingia kwenye bifu baada ya kudaiwa walikuwa wanamgombea pedeshee mmoja wa mjini, kila mmoja akijipa uhalali wa kumilikiwa.
Tukio hilo bichi kabisa lilitokea Juni 16, mwaka huu, Mikocheni jijini Dar es Salaam ambapo chanzo kinasema, wadada hao walikuwa wakirekodi sinema ambayo haijajulikana jina lake.
“Ni kweli walikuwa wakirekodi filamu, lakini kuna muda walizinguana ila watu wanasema bado wanakasirikiana kutokana na ile ishu ya kunyang’anyana mwanaume



Joti (Lucas Mhuvile – yule komediani wa Kundi la Orijino Komedi) alikuwepo eneo la tukio na ndiye aliyewapatanisha,” kilipasha chanzo hicho.
Joti alipotakiwa kuzungumzia ishu hiyo, alikiri kutokea lakini kwenye kurekodi filamu huku akikataa kufafanua.
“We’ jua kuwa ilikuwa filamu, si ugomvi serious,” alisema Joti.
Lulu hakupatikana kuzungumzia ishu hiyo lakini Husna alipopatikana alisema: “Tulitofautiana kikawaida tu kama wanawake lakini hatukufika kwenye mambo ya kupigana.”



No comments: