Friday, June 20, 2014

MANENO YA DIAMOND JUU YA WEMA SEPETU NA UJAUZITO

HAYA NDO MANENO YA DIAMOND ALIYOJIBU ALIPOULIZWA JUU YA UJAUZITO WA WEMA. Nasibu Abdul ‘Diamond’ alisema: “Unajua sisi tunaishi kama mke na mume kwa hiyo ishu ya mimba inawezekana lakini muongeaji ni Wema, mimi nataka iwe sapraizi.”
             









Wema amekanusha uzushi kwamba ana mimba, kasema hana, jana Wema alimjibu mdau mmoja kwenye social media kwamba, kwanini wanamlazimisha azae, mara wengine wanamwambia hazai ndo maana mpaka sasa ashiki mimba, Wema akawa kajibu kwamba atoae motto ni Mungu iweje wenyewe wakalie kumlazimisha azae.


JAMANI WADAU MNAOMLAZIMISHA HUYU BINTI ABEBE MIMBA, HIVI MKO DINI GANI? MAANA NIJUAVYO MIMI DINI ZOTE MBILI ZINAKATAZA MTU KUZAA NJE YA NDOA, SASA WEMA NA DIAMOND NI WACHUMBA ILA BADO HAWAJAOANA, SASA MNATAKA WEMA ABEBE MIMBA NJE YA NDOA? MSUBIRINI KWANZA AKISHAFUNGA NDOA NDO MUANZE KUMUULIZA, PIA JAMBO LA MTOTO NI MIPANGO YA WATU WAWILI JE LABDA WAMEAMUA HATA WAKIOANA WASIZAE KWANZA MPAKA WATAKAPOFIKA NGAZI FLANI YA MAFANIKIO, tusimkoseshe raha binti wa watu kwa maneno yasiyoyamsingi, umri wake bado unaruhusu sio kwamba anamiaka 40 hapana, na pia bado ni mchumba hajawa mke kwa hyo subirini awe kwenye ndoa ndo mumuulize kuzaa.

No comments: