Monday, October 27, 2014

TYRESE GYBSON WA HOLLYWOOD AKWAA SKENDO KUBWA.


Baby Boy
Huyu dada anaitwa TARAJ P. HENSON, yeye pia alicheza kama kinara wa kike kwenye hii movie, yeye ndie aliyekua girlfriend na baby mama  namba one wa Tyrese,


Hii movie inaitwa BABY BOY, na staring wa hii movie ni huyo kaka mweusi mwenye kipara anayeitwa TYRESE, movie hii ilitoka mwaka 2001 na ni movie ambayo ilimtoa huyu Tyrese, hii movie inapendwa sana na watu mpaka leo maana tyrese aliweza kuvaa uhusika haswa, maana nzima ya hii movie ni kuhusu kijana wa kiume ambaye pamoja na kwamba ameshakua mkubwa na ameshawazalisha mabinti kadhaa hapo mtaani lakini bado anaishi kwa mama yake na anadeka bado kama motto mdogo kwa mama yake , ndo maana ya BABY BOY. sasa bwana hivi majuzi kuna comedian mmoja wa huko huko Marekani anametoa mpya kwa kusema kwamba eti TYRESE alifanya vitendo vya kishoga na producer ndo maana akapewa nafasi ya kucheza hii movie ya BABY BOY, lakini madai hayo yamekanushwa vikali na TYRESE mwenyewe kwa kusema kwamba hajawahi kufanya vitendo kama hivyo na amempa kitisho comedian huyo anayechipukia kwamba atahakikisha hafanikiwi hao Hollywood,

MI NILIJUA HIZO KASHFA ZA KUTOA KITU FULANI KWA DIRECTOR AU PRODUCER ILI UPATE NAFASI YA KUCHEZA MOVIE IPO BONGO TU KUMBE HADI HOLLYWOOD, LAKINI KWA HOLLYWOOD NI MARA CHACHE SANA KUSIKIA UPUUZI KAMA HUU.

USHAURI WANGU KWA MADIRECTOR NI HUU....MCHEZESHE MTU MWENYE KIWANGO KIZURI ILI MOVIE YAKO IUZIKE NA IPENDWE, USIMCHEZESHE MTU KWASABABU UMETEMBEA NAE KWANI MWISHO WA SIKU NI UNAJIARIBIA KAZI MWENYEWE MANAKE UTAKUA UMEMCHEZESHA MTU ASIYENAKIWANGO.





No comments: