Wednesday, October 29, 2014

KWA WALE WAPENZI WA TOM CRUZ HII MOVIE SI YA KUKUPITA, EMBU WACHEKI PIA NA WAHINDI WALIVYOMUIGA TOM CRUZ.

Image result for bang bang 2014

Hii apo juu ni movie ya kihindi inaitwa BANG BANG, ni bonge la movie na staring wake handsome kweliweli anaitwa RITHIK ROSHAN, basi hii movie ni ya action , lakini story ya hii movie wameichukua kwenye movie iliyochezwa Hollywood na TOM CRUZ ambayo inaitwa NIGHT AND DAY.

                                                        RITHIK ROSHAN

Image result for hrithik roshan
Huyu Rithik Roshan wengi wanamtambua kwa jina la KRISH kwani movie iliyomtambulisha kwenye ulimwengu wa movie ni movie iliyokua inaitwa KRISH , na mrembo wetu IRINE UWOYA nae aliamua kumpa mwanae jina la KRISH kutokana na mapenzi ya hiyo mivie ya KRISH , anyway huyu kaka ni actor mkubwa huko India lakini pia baba yake ni actor na producer mkubwa sana kwa hiyo kijana karithi kazi ya baba yake.


                                                TOM CRUISE MOVIE NIGHT AND DAY

Sasa hiyo movie ya kihindi hapo juu ndo walichukua story kutoka kwenye hii movie, jamani jamani yani hii movie ya KNIGHT AND DAY ni bonge la movie kama mnavyomuona staring ni Tom akiwa na mwanadada CAMERON DIAZ pembeni na hawa walishawahi kuwa wapenzi kipindi cha nyuma, basi ndani ya movie hii kuna action za kutosha yani Tom anakinukisha humu jamani , na pia inavichekesho vya hapa na pale, technologia iliyotumika ni ya hali ya juu, yani hii ni aina ya movie unayoweza kuiangalia hata mara kumi.
 
TOM CRUISE NA CAMERON DIAZ
 
KAMA HUJAWAHI KUIANGALIA HII MOVIE NA WEWE NI MPENZI WA MOVIE ZA HOLLYWOODA BASI ITAFUTE UITAZAME YANI HUTAICHOKA.
 

 

No comments: