Saturday, August 23, 2014

STORY KUBWA YA LEO NI KUHUSU MREMBO JACKLINE WOLPER KUTAKA MTOTO...









Kwenye moja ya magazeti ya leo kuna story kwamba muigizaji mrembo na mwenye macho mazuri kuliko waigizaji wote Bongo eti anasaka motto, gazeti hilo linasema eti Wolper ametafuta motto bila mafanikio mpaka kuhofia kua huenda hazai, na kinachomfanya asake motto ni kutokana na maneno ya bibi yake aliyomwambia kwamba amzalie kitukuu hata akishindwa kulea ampelekee yeye atalea (huyu bibi wolper kama bibi yangu yani) maneno hayo eti ndo yamemfanya Wolper kuzidi kupata chachu ya kutamani motto.




HIVI HII HABARI NI YA KWELI? MANAKE SIKU HIZI MAGAZETI YANALALAMIKIWA SANA KWA KUTUNGA HABARI, HATUJAWAHI KUMSIKIA WOLPER AKIONGELEA SWALA LA KUTAKA MTOTO SEHEMU YEYOTE ZAIDI TUMEWAHI KUMSIKIA AKIONGELEA NDOA MARA KWA MARA ANAPOKUA KWENYE MAHUSIANO.

No comments: