Thursday, November 28, 2013

JACKLINE WOLPER........mmmhhhhhhh



Hii ni video inayoonyesha mahojiano kati ya muigizaji mrembo wa Tanzania Jackline Wolper na muandishi wa habari, kwenye haya mahojiano, Wolper amefunguka kuhusu maisha yake na baadhi ya wanaume aliowahi kutembea nao, katika list hiyo yumo Aly Kiba ambae ni mwanamziki, Jux ambaye pia ni mwanamziki, Diamond ambae pia ni mwanamziki pamoja na Dalas ambaye ni mfanyabiashara, Wolper pia amekiri kwamba anayempenzi ila hawezi kumuweka wazi kutokana na yaliyomkuta kwa Dalas, kwanza kabisa huyo mpenzi wa sasa anajisikiaje Wolper anavyoorodhesha wanaume aliowahi kua nao, huku akielezea jinsi alivyowapenda, na kwenye maelezo kuna mapungufu mengi mwenye akili anaweza kumsoma Wolper ni mschana wa aina gani kupitiaa mahojiano hayo, inawezekana huyo mpenzi wa sasa hana neno na haya maelezo, ila kubwa kuliko ni kwamba, zamani Diamond kipindi hicho ndo alikua anaanza kutoka kimziki aliwahi kukiri kua alikua na mahusiano na Wolper, tuhuma ambazo Wolper alizikataa na kusema maneno ya kashfa sana, miaka imeenda na sasa Diamond ndie mwanamziki pekee anayelipwa fedha nyingi Tanzania, na  ndo mwanamziki namba moja kwa sasa hapa nchini na licha ya hivyo Diamond hivi sasa anapesa ndefu kidogo, sasa kinachoshangaza ni jinsi Wolper alivyokiri hivi sasa kwamba alishakua na mahusiano na Diamond, swali, je amekiri kutokana na mafanikio aliyonayo Diamond hivi sasa? kwamba na yeye ataonekana yumo? manake kama mwanzo alimkashifu ni nini kimemfanya akubali sasa hivi? swali lingine, je Diamond angekua choka mbaya bado Wolper angekiri kwamba alishakua na mahusiano naye au bado angemkashifu? NI HAYO TU.

No comments: