Tuesday, November 26, 2013

ANGELINA JOLIE AFANYA KUFURU

huyu ni mwanamama muigizaji wa Marekani anaitwa Angelina Jolie na wa pembeni ni mumewe anaitwa Brad Pitt ambaye pia ni muigizaji mahili. na ukitaka kuona movie yao ya pamoja inaitwa MR&MRS SMITH.
basi inasemekana Brad anatajarijia kusherehekea siku yake ya kuzaliwa hivi karibuni, na mkewe akaamua kumsuprise kwa zawadi matata, manake ukiangalia hawa wote ni matajiri wa kutosha kwa hiyo wakitaka kununuliana zawadi ni lazima zawadi iwe ya tofauti ukizingatia wanauwezo wa kununua chochote duniani.

basi ma girl Angie akaamua kumnunulia mumewe hichi kisiwa ambacho bei yake ni dola million 20, unaambiwa kisiwa hichi kiko very private, kwenye hichi kisiwa kuna jumba zuri linaloweza kukufanya ujisikie hauko duniani uko peponi, hizo hapo chini ni baadhi tu ya picha za jumba hilo linavyoonekana kwa ndani.




haya na WEMA sijui atamnunulia nini Diamond ikifika birthday yake.

No comments: