Friday, May 9, 2014

KUHUSU WEMA SEPETU NA IN HER SHOES




Muda si mrefu Wema alikua anahojiwa chanel 5 na kama kawaida watu wengi walikua wanataka kujua hatma ya show yake ya in my shoes ambayo huwa inaonyeshwa kila jumatano kwenye kituo hicho cha tv lakini week mbili hizi show hiyo haijaonyeshwa hivyo watu wamekua wakihoji kulikoni na wengine wasiompenda wamekua wakisema kaishiwa ndo maana show haionyeshwi, Wema kasema kwamba kama ilivyo kawaida ya show nyingi kwenye luning zina seasons, hivyo basi show yake imesimama kwasababu season 1 imeisha na sasa ni maandalizi ya season 2, kwenye nilichokipenda ni hiki,
Bidada Wema kasema kwamba, season 2 mchumba wake Diamond nae atakuwepo kwenye show, mnanipata lakini, yani KAMA KIM ALIVYOMFANYA KANYE WEST AONEKANE KWENYE KEEPING UP WITH THE KARDASHIANS, ndo hivyo na sisi tutakavyomuona Kanye wa bongo kwenye show ya Kim wa Bongo, na pia kasema kutakua na marekebisho mengi ambayo yataifanya show inoge zaidi


mawazo ya kichwani kwangu....HIVI NDO TUTAKUA TUNAONA JINSI WEMA NA DIAMOND WAKIWA PAMOJA NYUMBANI, MALOVEY DOVEY TUNAYOYAONA KWENYE MAPICHA SASA HIVI TUTAKUA TUNAYAONA LIVE BILA CHENGA, UWWIIIII HII SI YA KUKOSA.

3 comments:

Anonymous said...

uwii hii siyakukosa kweli omg naisubiria sana

Anonymous said...

yeuwiiiiii wataniua hawa na mahaba yaoo jaman mieee.nawapendraaaaa adi naumwa

Anonymous said...

Natamani iwe hata kesho jamani!!!