Tuesday, May 27, 2014

MSIBA WA RACHEL HAULE, WEMA SEPETU NAE ABEBESHWA LAWAMA ZAKE.

                                           MAREHEMU RACHEL HAULE
Rachel Haule alikua ni muigizaji wa Bongo movies aliyejipatia sifa na umaarufu kwa uigizaji wake mahiri kwenye movie alizochewahi kucheza, inasemekana amefariki na kifo chake ni kutokana na kujifungua kwa operation, inasemekana kwamba, akiwa hospitali alifanyiwa operation kwa ajili ya kumtoa motto lakini kwa bahati mbaya motto akafariki na yeye akiwa kwenye hali mbaya hivyo akapelekwa chumba cha wagonjwa mahututi ICU, lakini muda si mrefu na yeye pia akafiriki, HAKIKA RACHEL ATAKUMBUKWA SANA HASA KWA USHIRIKIANO MZURI ALIOKUA NAO KWA WASANII WENZAKE, MUNGU AILAZE ROHO YAKE MAHALI PEMA PEPONI. 

WEMA SEPETU
Kufuatiaa msiba huo wasanii wa kike kwa wakiume asubuhi hii wamekua busy kuelezea hisia zao juu ya marehemu na wengi wamesimama hata kupost mambo yao binafsi na kuamua kupost habari za msiba na picha za marehemu huku wengine wakiulizwa maswali na mashabiki juu ya kifo cha marehemu na wamekua wakiwajibu mshabiki, wengi wa wasanii hao ni pamoja na Shilole, Snura, Irine Uwoya, Jackline Wolper, Steve Nyerere, Riyama, Lulu Michael na wengineo,

KASHESHE LILIANZA PALE BEAUTFULL ONYINYE WEMA SEPETU YEYE ALIPOAMKA NA KUPOST PICHA YA PERFUME ZAKE ALIZONUNUA NA KUELEZEA JINSI ANAVYOPENDA PERFUME NA JINSI ANAVYOTUMIA HELA NYINGI KUZINUNUA, mashabiki wakaanza kumuandama kwa maneno kwamba Wema huwa hajali misiba na kwamba wakati wenzake wanahuzunika juu ya marehemu yeye anapost perfume, wakasema kwamba hata alipofariki marehemu Adam Kuambiana ilikua hivyo hivyo eti Wema alianza kupost mengine baadae ndo akaanza kupost habari za msiba baada ya kusemwa.

WEWE UNAONAJE?


No comments: