Tuesday, May 6, 2014

KAMA PENNY BADO ANAMSUBIRI DIAMOND KWA MPANGO HUU MHH



Kwenye hii interview Penny wa watu alijielezeaga vizuri sana, ila watu wengi hawakupenda pale aliposema wamepeana nafasi na Diamond, yani watu walisema inamaana kama anasema wamepeana nafasi manake bado anategemea baadae Diamond kurudisha uhusiano na wengine kusema bado moyo wake haujakubaliana na kuachwa na ndo maana bado anaambatana sana na dada zake Diamond, wengi naona kwenye mitandao wanamshauri a move on,ila kwa mimi ninavyoona namuona kama ka move on na anafuraha na maisha yake, kaka bado kwa mpango huu hapo chini inabidi utoke ndukiii




                 DIAMOND NA WEMA MAHABA NIPINDUE KAMA VIATU VYA VANESA MDEE



Yani kama mnavyomuona hapo Wema na Diamond wanamambo mengi sana wanayoendana, licha ya kuwa wapenzi wanaweza pia wakafanya kazi pamoja,kama unavyomuona Wema kakamata mic hapo na kesho ukawii kusikia Diamond ana act movie na hivi yeye anamovie yake anayo actigi isiyo isha mpaka leo. pia licha ya hivyo Diamond akiwa na Wema unawaona kabisa hawa watu ni marafiki wanacheka na kutaniana kitu ambacho ni tofauti na Diamond akiwa na mpenzi mwingine mara nyingi hata kwenye picha BODY LANGUAGE HAZISOMI.

                                DIAMOND ALIPOPOKEA TUZO JUZI AKIWA NA MUCHUMBA WAKE



Haya licha ya kua they have a lot in common kuna hili la Diamond kupata mafanikio sana akiwa na Wema kuliko akiwa na demu mwingine yoyote duniani, sasa hapa kama Penny atamsubiri D sidhani kama atarudi manake hawezi kumwacha Wema ambaye anamfanya anyakue tuzo saba na kurudi kua na mschana ambaye kipindi yuko nae alipata tuzo moja.



Kingine kuna picha imepigwa juzi Wema na Diamond wako kwa mama Diamond wamepeleka zile tuzo saba, sasa hapo Penny hata kama mama mkwe anakupenda lakini anampenda zaidi mwanae na hawezi kamwe kuangalia mwanae akishuka anapenda mwanae awe juu na kama anaona mwanae yuko juu akiwa na Wema obviously itabidi akubali matokeo(nionavyo mimi hapo) ,kingine pamoja na kwamba wimbo wa NGOLOLO Diamond aliutoa akiwa na Penny lakini shukrani zinatolewa kwa mama yake na kwa Wema Penny hatajwi hata kwa mbali japo im sure Penny alishiriki hata kidogo kwenye swala la mawaidha, hapo ndo unaona kabisa jinsi Diamond alivyokolea kwa Madam, beautfull onyinye queen wa Bongo movies.



Diamond ndo msanii wa kiume pekee mwenye mashabiki wengi Tanzania na Wema ndo msanii wa kike pekee mwenye mashabiki wengi Tanzania, wakiungana maanake wanashare mashabiki kwa hyo chochote atakachokifanya mmoja wapo lazima ashinde labda hilo shindano wasiwekwe hawa wawili. kwa nionavyo mimi Penny hapa hana chake kama mashabiki wanavyosema instagram kwamba penny bado anamsubiri Diamond ni bora achape lapa kama ameshamove on tunamtakia maisha mema manake she is smart and beautfull too.

2 comments:

Anonymous said...

Dah yaani atasubiri sana,poor penny!yaani dai kuwa na penny alikuwa anarevenge baada yakuwa na ck,ila baadaye wote wakagundua wanajiumiza roho zao kwakuwa na watu wasiowapenda na kuamua kurudiana,sasahv ni mapenzi moto kwenda mbele.i am out

Unknown said...

Huhuhuuu,umesema vizuri rachel,ushauri wangu kwa Penny bora aachane na dada zake Daimond coz anazidi kujiumiza tu japo uson twamuona ana furaha,we have experience bana,anajikaza tu ila anaumia sana na kukosa usingizi akae mbali na mawifi wa ex wake mbona kitu cha kawaida tu,siamin kama esma na halina na queendareen hawata msapot kaka yao akitaka kuoa atakuja kuwaona wanafki kumbe ni haki yao kumsapot ndugu yao!ningekuwa yeye ningekaa hata mbali na social netwrks!napita tuu jamani