Friday, May 30, 2014

JACKLINE WOLPER KATISHERRR SANAA KWENYE HILI....

Tayari ipo sokoni
Hii movie hapo juu inaitwa Tom Boy, yani huwa Napata uvivu kuziangalia movie zetu za bongo kwasababu waschana mara nyingi wanaringaringa badala ya kuigiza kwa hiyo huwa naangalia movie za Wema Sepetu na JB tu kwasababu huwa naona wako real... LAKINI JANA NIMEBADILI MAWAZO, JAMANI NIMEANGALIA HIYO MOVIE HAPO JUU YA TOM BOY, YAAANI JACKLINE WOLPER KAJUA KUITENDEA HAKI NAFASI YAKE JAMANI, YANI WOLPER SIKUJUA KAMA UNAWEZA KUKAMUA KIASI HIKI.

WOLPER AKIWA JIKE


PICHA YA CHINI WOLPER AKIWA DUME

Yaani kwa mtu asiyemjua Wolper akaona hiyo movie angesema Wolper ndo yuko vile kumbe bidada kajua tu kuvaa uhusika, yani mapozi sasa ya kiume kabisa, ile sauti sio nzito lakini alijua kuikaza balaa, mi mwanzoni nilijua ataforce sauti ya kiume ili nije nimchambe lakini hakuforce kuongea kwa sauti nzito aliongea sauti ya kawaida ila iliyokua imesimama, sasa kwenye kimtia VITASA mshenga ndo nilikua hoi, na sehemu nyingine iliyoninoga ni pale DUME JIKE WOLPER lilipopewa habari kwamba lina ujauzito, uwiii Wolper aisee umetisha mbaya yaani acha wakuzushie msagaji maana kwa jinsi ulivyokamua mule lazima wengine wahisi yale ndo maisha yake, ni kama bi mwenda alivyokamuaga kwenye uchawi mpaka akitembea wakawa wanamzomea wanamuita mchawi.

Sehemu nyingine niliyoipenda ni jike dume lilivyomwambia mama yake aache vyombo vitaoshwa na mkwe mama akajua mkwe atakae kuja ni mwanaume kumbe jike dume linazungumzia demu mwenzake, Muhogo mchungu na Mama mashaka kama kawa wale ni siwezi hata kuwapima uigizaji wao manake wale ni wakaree wa toka Enzi, na MSHENGA nae noma balaa, Jackie nimekupenda sana kwenye hii movie,

HONGERA SANA MTUNISY MAANA WEWE NDO MWANDISHI WA STORY BONGE LA STORY NA ULIKATA KIU YOTE HASA ULIVYOAMUA KUTUONYESHA MPAKA KWENYE MAISHA YA NDOA YA JIKE DUME.



1 comment:

Anonymous said...

msgaji huyu hana lolote na analijua hilo wolper gambe msagajiiiiiiiiiiiii