Saturday, October 12, 2013

UNAMKUMBUKA HUYU?

Nadhani wengi wanaijua movie ya Africa kusini iliyokua gumzo miaka ya 90 movie ya SARAFINA. basi yule aliyecheza kama SARAFINA ndo huyu. jina lake halisi anaitwa lELETI KHUMALO alizaliwa mwaka 1970, ni mzulu, amecheza movie kama SARAFINA na HOTEL RWANDA.


                                                           LELETI KHUMALO AU SARAFINA
 
Picha hii ya chini ndio SARAFINA anavyoonekana sasa, bado mrembo vile vile


                                               LELETI KHUMALO AU SARAFINA
 
Hapa kwenye picha ya chini ndo cover la movie ya sarafina, hapo akiwa na mwigizaji bei mbaya wa Hollywood WHOOPI GOLDBERG. kumbuka kwamba kwenye movie licha ya Whoopi kuwepo, pia MIRIAM MAKEBA ambae ni marehemu sasa nae alikuwepo pamoja na DUMISANE.
 
 
                                                      SARAFINA NA WHOOPI GOLDBERG
 
Sarafina aliolewaga na msanii mwenzake aliyeigiza nae kwenye hii movie lakini waliachana inasemekana yule mwanaume alikua na uhusiano na wanawake wengi na pia alishakua na uhusiano mpaka na marehemu BRENDA FASIE. lakini sasa sarafina ameolewa tena na mfanya biashara maarufu wa huko South, na hii picha hapa chini ni ya siku ya harusi yao mwaka jana.
 
 
                                              SARAFINA NA MUMEWE SIKU YA HARUSI.
 
hayo ndo maisha ya muigizaji huyu aliyejizolea umaarufu mkubwa sana Enzi za miaka ya 90, Enzi hizo kila motto alikariri nyimbo za kwenye movie ya sarafina, na wengine mpaka step za kucheza walikariri, movie classic kama hizi ntakua nakuletea mara kwa mara ili tukumbukie Enzi.

No comments: