Monday, April 21, 2014

WEMA SEPETU NA GAZETI LA IJUMAA MAMBO SHWAAARIII.

Baada ya Wema kwenda kwenye ofisi ya gazeti la ijumaa kufanya fujo, kwa kuandikwa vibaya yeye na mpenzi wake, Wema kama mnavyomuona kwenye picha hapo chini akiangua varangati huku akiwa ameshika viatu mkononi, alishikwa na hasira hasa ikizingatiwa habari iliyoandikwa kuhusu mpenzi wake picha zilizotumika alizipiga Wema mwenyewe lakini waandishi wakazichukua na kuzitumia vibaya, anyway shuka chini nikujuze.
                                    WEMA SEPETU







Jana siku ya Pasaka Wema amepokea tuzo ya kua sexiest girl wa gazeti hilo hilo alilogombana nalo.
                     WEMA AKIWA NA TUZO

Wema kawapiga chali wakina Jokate na Wolper kwenye kinyang'anyiro hicho, TUNALIPONGEZA GAZETI HILI KWANZA KWA KUMTUNUKU WEMA TUZO HIZO PIA HAPA INAONYESHA WAMEMSAMEHE WEMA KWA KUFANYA FUJO OFISINI KWAO LAKINI PIA WEMA TUNAMPONGEZA ZAIDI KWA KUTOKUWA NA KINYONGO NA KWENDA KUPOKEA TUZO HIYO.    kweli ule msemo wa ndugu wakigombana shika jembe na wakipatana shika kapu kavune ndo umejidhihirisha, hebu nishike kapu mie nikavune ubuyu.



2 comments:

mama boyy said...

Kwani global wamempa bure hiyo tuzo au ni kura za wananchi maana unavyosema ndugu wakigombana shika jembe ukalime it means wamempa ushindi ili kumaliza mgogoro wao heyyyy angalia unachoandika kinafikirika vipi sasa hivi status zako zinapoelekea utaharibu be reality usiongeze wala kupunguza

Anonymous said...

U better go to school first bcoz u don't know even how to write news