Wednesday, April 9, 2014

SHOW YA WEMA SEPETU EPISODE 19 TUICHAMBUE




Haya wapendwa jana ile show yetu tuipendayo ya Wema imewekwa kwenye mtandao na kwa ambao hawakuiona ndo hiyo hapo jionee .


Kwa maoni yangu, naanza kutiririka kama ifuatavyo, kwanza kabisa nianze na Wema mwenyewe, jamani Wema ni mschana mwenye moyo kama wa motto yani she is a sweet heart jamani, nasema moyo kama wa motto kwasababu hajui UNAFKI, yani Wema akimkasirikia mtu anaonyesha hapo hapo, kama hakupendi atakuonyesha, kama anakupenda atakuonyesha na atakupenda toka moyoni, ni bora kua na mtu wa aina hii kuliko na mtu anayekuchekea usoni wakati moyoni mh, turudi kwa KAKA MANAGER, bwana Martin ni wewe pekee unayemmudu Wema, ila linapotokea tatizo usishout wewe ndo unatakiwa kuhakikisha tatizo linasorvewa kiustaarabu bila majirani kusikia, sasa zamu ya TOTO PETIT MAN WAKUACHE. mi nakapenda haka katoto ka madam lakini kwa nilivyoona kwenye hii show motto inabidi ukue kiakili sasa, jamani dunia ya leo, kijana ambaye bado hana maendeleo yeye mwenyewe yani hana nyumba au kitegauchumi, kweli unaweza kutumia million nne kwa usiku mmoja, manake hapa madam alikua analalamika kampa Petit million nne na laki 8 asubuhi yake Petit hana kitu na kwa mujibu wa Martin Petit alikula bata sana usiku mpaka kuku wakazimia kwa wivu, sasa jamani hivi million 4 si inatosha kuanzisha biashara? kuliko hyo hela kulia bata tena hela si yako kwanini usingeizungushia kwenye biashara, mtamtegemea Madam mpaka lini? na kama mnafanya kazi kwa Madam namna hii hakuna atakaye ichukulia compuni serious manake nani atataka kuwekeza kwenye compuni ambayo mfanya kazi anakula hela tena bila uwoga.


                        NI HAYO TU





No comments: