Sunday, April 27, 2014

WANAOMUIGA JOTI MDEBWEDO SASA BASI JAMANI



Joti na kundi lake la ze comedy nafikiri ndo walifanya kitendo cha mchekeshaji kuvaa nguo za kike kishamiri kama zamani walikuwepo basi miaka ya hivi karibuni joti ndo kashamirisha zaidi. TATIZO LINAKUJA HAPA....................hivi, wachekeshaji wengine na wenyewe hawawezi kubuni jamani kitu kingine zaidi ya wenyewe pia kuvaa nguo za kike na kujiremba na kuanza kuchekesha, kwa Joti ilikua inachekesha, sasa walivyovamia wengine imekua si kichekesho tena bali ni kero, kila mchekeshaji utamuona kavaa nguo za Kike halafu anakua anatangaza taarifa ya habari, JAMANI? hii kali na inachosha, HAYA SASA WAKINA JOTI KAZI KWENU KUBUNI KITU KIPYA ILI MUWEZE KUWAVUTIA WATAZAMAJI WENU. NA KWA WALE WANAOWAIGA BADILIKENI ILI TUVUTIWE NA STYLE ZENU NYINYI KAMA NYINYI LA SIVYO MKIENDELEA KUIGA HAKUNA MTU ATAKAYE WAPA ATTENTION .

No comments: