Sunday, January 5, 2014

MASHAUZI KAMA YA BONGO MOVIE YAMUUMBUA HUYU MUIGIZAJI WA NIGERIA

                                        
                                                          CHIKA IKE




Huyu dada ni muigizaji kutoka Nigeria, anaitwa Chika Ike, mwanadada huyu inasemekana amekua akipenda sana maonyesho ya mali zake na kila anachofanya lazima akiweke wazi, sasa kwa mwaka jana tu naskia kaenda vacation mara tatu nchi tofauti tofauti, kubwa kuliko ni hivi majuzi ambapo kasambaza picha kwenye mitandao ya kijamii akijielezea kua yuko vacation huko ABU DHABI, na kwenye picha hizo anasema kafikia kwenye moja ya hotel za bei mbaya duniani inayoitwa EMIRATES PALACE HOTEL iliyopo huko Abu Dhabi, unaambiwa kulala hapo ni kuanzia dola 5000 mpaka 17000 kwa siku, sasa kilichofanya watu wamchambe mwanadada huyu ni kwamba, kwenye picha zote kama mnazoziona hapo juu hakuna picha hata moja aliyoonyesha labda yuko chumbani kama ambavyo hufanya akiwa kwenye hotel nyingine, kitu ambacho kimefanya watu wamseme kua ni muongo alienda tu hotelini hapo kupiga picha ili awalingishie wenzie, wamesema sehemu alizopigia picha mtu yoyote anaweza kuingia na kupiga picha, mashauzi haya huwakuta dada zetu wengi wa bongo movie, mfano kama Jackline Wolper alivyoringishia gari kumbe la kuhongwa na mwisho wa siku likachukuliwa,

No comments: