Monday, December 23, 2013

WEMA SEPETU AWA MU AFRICA



Hapa kuna picha inayomuonyesha muigizaji namba moja, nasema namba moja kwasababu yeye ndo muigizaji pekee wa kike anayeuza magazeti, yani habari ya huyu dada ikitoka lazima isomwe hata kama utafumba macho bado utaisoma tu, haya nirudi kwenye mada, hii ni cover ya magazine ya hapa Bongo inayoitwa VIBE, na toleo jipya wamemtoa Wema Sepetu, kwa wanaomjua Wema, wengi tunajua anarangi ya mwili kama ya mzungu yani ni mweupe sana, lakini kwenye hii picha wamemfanya Wema kua mweuzi kama mnavyoona, na pia hawajampigisha pamba, wamemvisha kanga, vazi la kinamama wa kiafrica na majani majani, wengi wametoa maoni yao na kusifu picha hii japo wengine wamesema u fake ulizidi sana.

No comments: