Wednesday, September 18, 2013

OPRAH WINFREY ALEGEZA MSIMAMO

Mwanamama bilionea Oprah Winfrey wa Marekani kaamua kulegeza msimamo wake juu ya nini kionyeshwe kwenye television yake inayoitwa OWN. unaambiwa tv ya Oprah ilikua inaonyesha vipindi vile vya kuhamasisha tu kitu ambacho kilifanya Tv hiyo kua na watazamaji wachache na idadi ya watazamaji kuelendelea kupungua kila siku. Oprah ameamua kuanza kuonyesha vipindi vya kuchangamsha pamoja na reality shows, na vipindi hivyo vinatazamiwa kuongeza idadi ya watazamaji.
 
Najua wengi wenu mtashangaa kwanini nimemuweka Oprah humu kwenye blog ya movie, ni kwamba Oprah pia ameshacheza movie kadhaa, blog hii itakua inamfwatilia mtu yeyote yule anayecheza movie hata kama mtu huyo ni mwanamziki, doc, mwalimu, au mtangazaji, ili mradi tu ucheze movie basi wewe utakua na uhalali wa kuwekwa humu.

No comments: