Monday, September 23, 2013

FAST AND FURIOUS 7 INATOKA MWAKANI, UNAJUA NANI ATAKUWEPO NA NANI HATOKUWEPO?

Naimani kwa wale wapenzi wa movie mmeshaona movie za fast and furious, zipo part one mpaka six, hii six ndo ilitoka mwaka huu na ikawa gumzo midomoni mwa watu. sasa FAST AND FURIOUS 7 ipo jikoni.
Movie hii inayotarajiwa kutoka july mwakani, imeandikwa na Chriss Morgan na director wake ni James Wan. Mwezi huu wa tisa ndio movie hii wameanza kui shoot, humo ndani watakaokuwepo ni Vin Diesel, Paul Walker, Dwayne Johnson, Tyrese Gibson, Jason Stantham na Lucas Black.


hapo kwenye hii picha anaonekana vin Diesel na Justin Beaber, wengi walijiuliza kulikoni Justin awepo kwenye trailer ya Fast n furious 7? jibu ni kwamba hyo trailer sio official, Justin hatokuwepo kwenye hii movie, ila Justin kwa jinsi anavyotuhumiwa kukimbiza magari yake huko Marekani angependeza sana kukimbiza magari na kwenye hii movie pia.

 
Hapo chini ni picha ya muigizaji kutoka India ( Bollywood) anaitwa Deepika Padukone, huyu kwenye fast n furious six alikuwepo lakini kwenye 7 hatokuwepoo kutokana na kua na ratiba ya kucheza movie na Shuhrukh Khan inayoitwa Happy new year, kutokana na fast nn furious 7 kurekodiwa haraka yani haijapishana sana na fast n furious 6 ndo maana imemuwia vigumu Deepika kuwepo.
 
                                                      DEEPIKA PADUKONE
 
Kwa mnaompenda Jason Stantham basi naye safari hii atakuwepo kajaa tele, jamaa huyu naye mkali sana wa movie za action

 
kama kawaida police lazima awepo kulinda amani,  huyu ni Dwayne Johnson huwa ana act kama police nafasi anayoimudu vilivyo. Jamaa kapanda halafu kajazia balaa yani jambazi akaimuona tu anasalim amri mwenyewe
 
                                                       DWAYNE JOHNSON

hawa kwenye movie huwa wanaukaribu sana majina yao ya kwenye movie ni Bryan na mwenye upara ni Torreto ila majina yao halisi ni Paul Walker na wa upara ni Vin Diesel

                                                      PAUL WALKER NA VIN DIESEL
 
 
 Ma meen Ludacriss nae kama kawaida ndani ya nyumba na kwenye sekta ya uongeaji pumba na vichekesho vya hapa na pale kama kawaida Tyrese Gibson kajaa tele.

                                          LUDACRISS NA TYRESE GIBSON
 
Ludacriss na Tyrese kwa wale wasiofahamu ni wanamziki pia.

No comments: