Friday, September 20, 2013

MASTAR HAWA WA BONGO MOVIE WAKIFWATA HAYA WATAKUA NA HADHI YA USTAR

Ningependa nianze na Aunt Lulu, huyu binti ni mrembo na anaumbile kubwa, ningependa nimlinganishe na Queen Latifa wa Marekani.

                                                          AUNT LULU

 
QUEEN LATIFAH

Kwanza kabisa ni ngozi, Latifah yeye ngozi yake ni laini na anarangi moja kuanzia miguuni mpaka usoni, endapo Lulu ataamua kushughulikia ngozi yake basi atazidi kua bomba. lakini pia ni aina ya mavazi, Lulu anaumbile zuri kuliko la Queen Latifa, lakini Queen anapendeza zaidi kutokana na choice ya mavazi yake, anavaa mavazi yanayofunika maumbile yake na yanayomkaa vizuri kuendana na umbile lake, pia make up yake huwa imetulia na urembo kama heleni na shanga pia zinaendana na nguo na havai urembo ukawa too much. kwa hiyo msanii wetu Aunt Lulu ukiweza tu kufwata haya hakika utakua juu kwasababu wewe ni mzuri wa sura mpaka umbo.

2. Wema Sepetu ningependa nimlinganishe na Tyrah Banks. kwanza kabisa wote warefu na na wanamaumbile ya kiafrika. na kwa msiofahamu Tyra pia hua anacheza movie na ameshacheza movie kama Halloween Resurrection na Love & basketball.

                                                   WEMA SEPETU



                                                              TYRAH BANKS
Hizi picha zinawaonyesha mastar hawa nyuso zao, Wema angependeza sana kama angejitahidi akawa na rangi ya mwili kama ya Tyra, yani rangi halisi ya Wema ya zamani ilikua kama Tyra, sasa Wema wetu akifanikiwa kuirudisha tu ile rangi atakua bomba kabisa, pia make up, ikiwa machoni utapaka eye shadow inayong'aa inapendeza mdomoni ukapaka lipstic ya mbali sanah ii inasaidia kukufanya usionekane shangingi. pia foundation nayo, inatakiwa ikipakwa kue na uhalisia,

 Tyrah akiwa kwenye red carpet,

 
na hapo ni Wema akiwa kwenye redcarpet, hua anapendeza sana wema na ni mzuri kwakweli, najua ikifika mahali akaamua kurudi kwenye ngozi yake original basi atawakosha wengi sana.

 
 3. Jokate pia kwa wale msiomjua ameshacheza movie kadhaa, napenda kumfananisha Joketi na Megan Good, huyu ni muigizaji wa marekani na amecheza movie kama Think like a man ambayo inatamba sana hivi sasa. mwanadada huyu na Jokate huwa wanaendana sana kuanzia style ya mavazi make up mpaka skin colour,
                                                             MEGAN GOOD

 Rangi ya Megan na Jokate zinafanana na zinapendeza kwakweli, wote wa brown, wote wanapaka make up zinazowafanya waonekane natural. na wote wana maintain miili yao vvizuri kiasi kwamba huwa hawanenepi hovyo.

                                                             JOKATE MWEGELO

 
MEGAN GOOD kwenye red carpet

 
JOKATE kwenye red carpet

 
MEGAN GOOD na mumewe ambaye ni pastor huko Marekani


Jokate anamuonekano wa kistar kabisa huwa sioni kasoro yake, ila tatizo ni kashfa tu zinazomuandama, angekua hana kashfa kwakweli angekua juu sana, muangalie Megan Good ni mzuri na hana kashfa kitu kinachomfanya azidi kuheshimika, na anamume wake na katulia. kwa hyo Jojo ukiweza kurekebisha hapo kwenye mambo ya makashfa tu utakua star wa ukwee.

No comments: