Wednesday, March 12, 2014

JACKLINE WOLPER AOKOLEWA NA KIKI FASHION. FASHION POLICE YAMUANGUKIA LEO



Hebu tumuangalie mwanadada mwenye mvuto wa pekee kwenye Bongo movie, huyu si mwingine ni JACKLINE WOLPER MASSAWE mchaga mwenzangu, she is very beautyfull we all know dat. lakini bwana FASHION POLICE leo imetua kwake. tumuangalie Wolper kipindi ndo anaingia kwenye GAMEEEE, kwenye sekta ya mavazi alikuwaje na sasa yukoje, jinsi unavyovaa ikumbukwe kwamba ndio mtu anavyouchukulia utu wako na kama wewe ni msanii basi ndo jinsi utakavyojitengenezea kazi au kujikosesha kazi. twende sasaaaa

                               JACKLINE WOLPER
Hapa mrembo yani ni kama kafungua duka la kuuza urembo mwilini mwake, yani kavaa vitu mia moja visivyo na ulazima, style ya nywele haileweki kama pia kafungua duka la kuuza nywele manake nywele za aina tatu ziko kichwani na zote mbaya, hebu niambie hizo rasta zafanya nini jamani, hizo nywele nyekundu hapo mbele Wolper kwanini unamuiga Rihana, hicho kibanio uwii jamani, yani kichwani huo mchanganyiko wa rangi ni kama rainbow. nguo siielewi, pete siielewi, herein, yani vinaeleweka lakini vilivyovaliwa kwa pamoja ni uchafu mtupu. hilo kolokolo kwenye funguo ya gari, simu kwanini usiweke kwenye pochi, hivi mmewahi kumuona msanii wa nje na masimu kwenye red carpet.
minywele myekundu jamani,

picha ya hapo chini, ni kama kabeba kuku mwekundu kichwani,
sasa bwana hizo picha za juu ni kipindi hicho long time ago wakati kaanza, hivi sasa yukoje, shuka na mimi daunnn

huyu hapa chini ndo Wolper wa sasa, binti anayejua kujipangilia nguo, binti anayejua umuhimu wa kwenye kwa designer na kuomba adisigniwe nguo, very classic to be honest, everythin on point, the hair, the make up, the shoes, amaizing.

speechless, kweli huyu motto wa kichaga, kwa huu muonekano hata Hollywood wanaweza kumpa kazi,
TUKO CHINI YA MIGUU YAKE, TUNAMUOMBA ASIJE AKAJISAHAU AKARUDI KUA HIVI KAMA HII PICHA YA CHINI.
NIMEMALIZERRRRR....................................................

No comments: